Katika aina hii ya mkopo, mwanachama ataweza kuchukua kiasi kisichozidi Shs. 30,000,000/=. Riba ni 1.5% kwa mwezi kwa njia ya riba punguzo (Reducing Balance Method). Marejesho ni kuanzia mwaka mmoja hadi miaka mitatu.
Mkopo huu ni kiasi kisichozidi Tsh 3,000,000/= Riba ni 2.0% kwa mwezi kwa njia ya riba punguzo (Reducing Balance Method). Marejesho ni miezi sita.
Mkopo huu ni kiasi kisichozidi Tsh 3,000,000/= Riba ni 2.0% kwa mwezi kwa njia ya riba punguzo (Reducing Balance Method). Marejesho ni kuanzia mwaka mmoja had miaka miwili.
Mkopo huu ni kiasi kisichozidi Tsh 100,000/= Riba ni 5.0% kwa mwezi. Marejesho ni mwezi mmoja. Mkopo huu hutolewa wakati wowote pindi mwanachama anapohitaji
Mkopo huu ni kiasi kisichozidi Tsh 100,000/= Riba ni 5.0% kwa mwezi. Marejesho ni mwezi mmoja. Mkopo huu hutolewa kwa sikukuu zinazotambulika kiserikali
UWSA SACCOS LTD ni Chama cha Ushirika cha Akiba na Mikopo kilichosajiliwa kwa namba 914MBR. Chama hiki kilianzishwa mahususi ili kusaidia watumishi waajiriwa wa Mamlaka ya Majisafi na usafi wa Mazingira Mbeya.
Chama hiki kina jumla ya Wanachama 148 ikiwa wanaume ni 88 na wanawake ni 60 wenye jumla ya Hisa zenye thamani ya Shilingi 62,315,000/=.
Hadi kufikia mwaka 2022, Chama kimekuza mtaji wake hadi kufikia Shilingi Milioni 350 ikiwa ni mjumuisho wa Hisa na Akiba za Wanachama.
Mamlaka ya Chama yanatokana na Sheria ya Vyama vya Ushirika Na. 6 ya mwaka 2013 na Sheria ya Huduma Ndogo za Fedha Na. 10 ya mwaka 2018 na Kanuni zake. Chama kilianzishwa ili kukuza maslahi ya kiuchumi ya chama na Wanachama
Dira ya Chama ni; Kuwa Chama bora cha akiba na mikopo chenye kutoa huduma bora na riba nafuu kwa Wanachama,...
Soma ZaidiDhima ya Chama ni; Kutoa huduma bora ya utunzaji wa akiba za Wanachama, kutoa mikopo kwa Wanachama na kutoa elimu,...
Soma ZaidiMisingi ni suala la muhimu wakati wa kusimamia shughuli za Chama kwani husaidia kufikia malengo ya chama,...
Read MoreKuhamasisha uwekaji wa akiba, hisa na amana ili kuendeleza na kukuza mtaji wa chama.
Kutoa elimu kwa jamii nzima ili kujua umuhimu wa kujiunga na UWSA SACCOS.
Kujengea uwezo Wanachama kwa kutoa mikopo yenye riba nafuu ili kuwainua kiuchumi.
Kutoa elimu kwa Wanachama ihusuyo bidhaa za Chama.
Soma Zaidi